LULU AFUTA AKAUNTI YAKE INSTAGRAM




Muigizaji wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’ .


MUIGIZAJI wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’ aliyekuwa na wafuasi wengi kwenye Instagram, ameamua kujiondoa baada ya kushambuliwa kwa matusi na baadhi ya watu kufuatia kifo cha mpenzi wake.
Kufuatia kifo cha kutatanisha cha Lusekelo Samson Mwandenga ‘Secky’, watu wengi walianza kumtukana Lulu wakimhusisha pia na kifo hicho huku pia wakiweka picha zinazomuonesha alipokuwa na marehemu.

Muigizaji wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’ .
Msanii mkongwe wa filamu, William Mtitu amefunguka na kuwataka watu kuacha kumshambulia Lulu kwa kitu ambacho hahusiki nacho.
Marehemu Lusekelo Samson Mwandenga 'Secky' enzi za uhai wake.