ALI KIBA AANZA ZIARA YA KUKUTANA NA MASHABIKI WAKE KWENYE DALADALA


Staa wa Muziki TZ ambae usiku wa June 13 2015 aliingia kwenye headlines kubwa baada ya kuibuka na ushindi wa jumla ya Tuzo SITA kuonesha jinsi ambavyo watu wake mtaani wamemkubali kwenye ujio wake mwingine baada ya kimya cha muda mrefu.

Ali Kiba ni mshindi pia wa Tuzo za Watu 2015kwenye nafasi ya msanii wa kiume anayependwa.. YES, niko nae leo tena.. kaingia zake mtaani na akaona njia poa ya kukutana na watu wake ni kuingia katika daladala na kupiga story na kila shabiki wake wa nguvu aliyekutana nae humo.


Safari ilianzia mitaa ya Kariakoo katikati ya Dar es Salaam.. alafu ikaenda mpaka Tandika, Temeke na mwisho kabisa ikawa maeneo ya Ilala.


















Na wewe unatamani kuwa karibu na staa huyu? Ishu iko hivi, Ali Kiba amesema kesho anaendelea tena, yeye na watu wake ndani ya daladala kituo kwa kituo, kwa hiyo kama wewe ni mtumiaji wa usafiri huu pia katikati ya Jiji basi huenda kesho ikawa siku yako pia mtu wa nguvu!!